SARAH K LISEME SONG

Saturday, April 7, 2012

MWILI WA MAREHEMU STEVEN KANUMBA KABLA YA KUINGIZWA MOCHWARI
Muigizaji wa filamu nchini Stephen Kanumba amefariki usiku wa kuamkia leo,baada ya ugomvi na mpenzi wake huko nyumbani kwake Sinza Vatican.Mpenzi huyo ametoroka na inadaiwa alimsukuma marehemu kwa nyuma na kudondokea kisogo.Kanumba alilalamika maumivu makali ya kichwa ambapo alimwuita mdogo wake ampeleke hospitali,lakini alifariki kabla hajafika huko.Mwili wake umehifadhiwa Muhimbili.Source: Radio One
Hii ndiyo sura ya ndugu yetu Steven Kanumba, mara baada ya kufikishwa hospitalini

 Nyumbani kwa marehemu
 MC Nova

 Ndani ya geti-nyumbani kwa marehemu

 Steve Nyerere aliyevalia Polo shirt ya mistari mweusi na mweusi

 Mwigizaji a.k.a Chopa Mchopanga (katikati)
 Msanii wa Bongo Flava, Noora wa tatu kutoka kushoto

 Mvua akinyesha, alkini watu bado wako msibani
 Gari la Marehemu Steven Kanumba
 Mwigizaji wa Bongo Movie aliyekuwa muongozaji wa magari na kutoa tahadhari kwa wapenzi wa marehemu
 Dogo akipigwa mvua kali

 Mjasiliamali, Dotnata aliyenyoosha mkono wake wa kulia akipigwa mvua msibani
 Mwigizaji a.k.a Judy akihojiwa Live Channel Five
 Watu hawaamini kifo cha Kanumba (jembe)
 Mwigizaji Johari akilia katika mahojiano na EATV
 Mwigizaji maarufu sana, a.k.a Ray aliyevalia kofia akiwasiliana na jamaa baada ya mahojiano na waandishi wa habari
 Nyumbani kwa Steven Kanumba



Blogger na Graphic Designer, Rulea Sanga (mwenye njano) akitafuta matukio kwaajili yako wewe mdau wa blogu hii

 Mkurugenzi wa Global Publisher, Erick Shigongo akishirikiana na watengenezaji wa hema.
 Ndani ya geti la marehemu Steven Kanumba


Blogger Rulea Sanga aliyevalia njano halkukosa msibani

H-BABA akihojiwa na waandishi wa habari
Wapenzi na ndugu wa marehemu Steven Kanumba nyumbani kwake
Mwigizaji Mainda wa pili kutoka kushoto akimfariji rafiki yake
Waigizaji wa filamu
Mwimbaji huyu alielezea jinsi alivyoaagana na Marehemu Steve Kanuba alipohudhuria katika bendi yake siku ya jana usiku, anasema  marehemu alimtania kuwa kesho ambayo ni leo kuwa atakuja na suti kali sana ambayo ameinunua katika bendi yake
Mjasiliamali Shigongo wa Global Publisher akihojiwa na waandishi wa habari, alisema ni kitu chema kufanya kazi yako kwa kumkumbuka Mungu
Ruge wa Clouds FM alisema, ni pengo kubwa sana kwani katika sanaa alikuwa anahitajika sana


HISTORIA FUPI YA MAREHEMU STEVEN KANUMBA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjGx1fkd0U4Wl-fwTYlgh2rwLehfofVqX_VSccGny9eU7IuNXJEGjp0AKelcLktaUpd10SZ3MR-NWwEITcIlW26fbaXcOvvbaYu6bksEcDY1urllPrxfAGAcMdwfqOs9LshO6-Lm5UT3J0b/s1600/Steve+Kanumba.jpg

HISTORIA YAKE:

Steven Charles Kanumbaa alizaliwa Januari 8, mwaka 1984 mkoani Shinyanga kabla ya umauti kumfiia Aprili 6, mwaka 2012.

Elimu ya msingi alipata katika shule ya Bugoyi, na baadaye akajiunga na sekondari ya Mwadui, kabla ya kuhamia Dar Christian Seminary.

Baada ya kumaliza Kidato cha Nne Dar Christian, Kanumba alijiunga na sekondari ya Jitegemee, Dar es Salaam pia kwa elimu ya Kidato cha Tano na Sita.

Ni ni wakati huo akiwa Jitegemee Kanumba alianza shughuli za sanaa katika Kundi la Kaole Sanaa Group la Magomeni, Dar es Salaam.

Baada ya kukomaa Kaole, Kanumba aliamua kuanzisha kampuni yake mwenyewe ya filamu na hadi anakutwa na umauti alikuwa mwigizaji anayefahamika Afrika nzima.

Ameshirikiana na wasanii wakubwa duniani kama Ramsey Nouah wa Nigeria na amefanya kazi na mastaa wengine kadhaa wa Nigeria.

Miongoni mwa filamu ambazo alifanya ni Dar To Lagos, She is My Sister, Ancle JJ, Oprah, Tufani, Johari, Gharika, Baragumu, Sikitiko Langu, Dangerous Desire, Cross My Sin, Village Pastor, Family Tears na kadhalika.

Hivi karibuni, alikaririwa akisema atagombea Ubunge katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2015.

Kanumba atakumbukwa na wengi sana kwa ucheshi wake- upole na ushirikiano mzuri na wenzake katika kazi.

Kifo cha Kanumba ni pigo katika tasniya ya filamu Tanzania. Taifa limempoteza mtu ambaye alikwishaanza kuitangaza vema nchi kupitia sanaa hiyo na ambaye angetarajiwa kuitangaza zaidi katika anga za kimataifa zaidi kupitia sanaa hii.

Nigeria sasa wanajua Tanzania sasa filamu. Nchi nyingi za Afrika zinajua sasa nah ii sehemu ya kazi nzuri kwa Kanumba.

Mwenyewe aliwahi kukaririwa alifika hadi Hollywood hadi Marekani, ambayo ni ‘makka’ ya wacheza filamu. Kwa sasa mwili wa marehemu upo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam.

Mungu aiweke pema peponi roho ya marehemu. Amin.

2 comments:

  1. Inaniuma sana kwakua Steven KANUMBA yeye ndo mtu wakwanza alie nisaidia kunifunza hatua zangu zakwanza kipindi arikuja jijini Bujumbura mwaka 2010 Kwenye kundi ramaigizo akiwa pamoja na dada Irene UWOYA.nitamkumbuka nduguyangu Steven Ch KANUMBA

    ReplyDelete
  2. Siku zote nikiona picha hii hua napata uchungu san, kwakua Steven Ch KANUMBA alikua msada kwangu. yeye ndie mtu wakwanza alie nifunza hatua zangu zakwanza kwenye kundi la sanaa Great Lakes jijini Bujumbura mwaka 2010 kipindi alikuja kupiga show pamoja nadada IRENE.MUNGU ailaze roho ya marehemu mahali pema.KANUMBA The great sito kusahau kwawema ulionitendea

    ReplyDelete