SARAH K LISEME SONG

Monday, July 30, 2012

MUME WA JACK ALILIA NDOA GEREZANI


MUME wa modo Jacqueline Patrick aliyepo nyuma ya nondo za Mahabusu ya Gereza la Keko, Dar es Salaam kwa tuhuma za kusafirisha mihadarati, Abdullatif Fundikira ‘Tiff’ ameililia ndoa yake akisema kuwa amegundua kuna watu wanataka kuivunja kwa makusudi.
Akizungumza tulipomtembelea gerezani hapo wikiendi iliyopita, Tiff alisema kuwa anashangazwa na watu ambao anawaheshimu kuwa ni shemeji zake na ni marafiki wa mkewe lakini wamekuwa wakipepeta umbeya juu ya ndoa yake ili tu ivunjike.
“Aisee inauma sana, lakini Jack hasisikilize maneno ya watu. Akumbuke tumetoka mbali na enzi ya kula bata kwani mimi nikikumbuka kuna wakati natokwa machozi na ukweli ni kwamba siwezi kukubali ndoa yangu ivunjike,” alisema Tiff.

No comments:

Post a Comment